Lebo

Ijumaa, 8 Julai 2022

DHANA YA AKILI NA MAFANIKIO

 SOMO LA KWANZA


*DHANA YA AKILI NA MAFANIKIO*


📙📙📙📚📚📚📚📙📙📙


Sehemu ya TATU 


*Ijue PREFRONTAL CORTEX; sehemu CHANYA ya Akili inayopambana na nguvu HASI (LIMBIC SYSTEM)*





Naendelea kusisitiza kuwa *Ametukuka Mwenyezi-Mungu; mbora wa kuumba*! Katika sehemu ya mbele ya ubongo wa mwanadamu; Kuna sehemu inayoitwa *Prefrontal Cortex*; hii ni sehemu CHANYA inayosimamia mafanikio makubwa ya mwanadamu. Ili kuifahamu vizuri sehemu hii ni vizuri tukajua upande HASI *(LIMBIC SYSTEM)*.


*LIMBIC SYSTEM*



Hii ni sehemu iliyo maeneo ya paji la uso. Huu ni mfumo hasi unaomfanya mwanadamu:

- Awe mvivu

- Apende starehe

- Asipende kujihangaisha

- Akate tamaa mapema

- Aghairishe Mambo muhimu

- Asione umuhimu kusonga mbele n.k.

Mfumo huu unazalisha kemikali iitwayo *Dopermine* (inayozalishwa na Amygdala)  ambayo humfanya mwanadamu Apende kuliwazwa na asipende kabisa kujituma. Umeshawahi kuona Alfajir unataka kuamka lakini kuna kitu kinakubembeleza na kukwambia uendelee kulala!? *Hiyo ndiyo kazi inayofanywa na Limbic system*. Hiki ni kilevi. Kwa bahati mbaya; mfumo huu Mwenyezi-Mungu Amauumba ukiwa kamili kwa 100% tangu Mtoto anapozaliwa!


*PREFRONTAL CORTEX*

Ili kudhibiti nguvu ya Limbic system; Mwenyezi-Mungu Ametuwekea sehemu hii CHANYA ya Prefrontal Cortex. Mfumo huu huwa hauko kamili kimaumbile; huwa inakuwa kadiri mwanadamu anavyojitahidi kupambana na nguvu HASI. Kwa hiyo; jinsi unavyozidi kufanya Mambo ya kimaendeleo na kujituma; mfumo huu unakua na Limbic system hupungua nguvu. Unapoweka malengo makubwa na kuanza kuchukua maamuzi makubwa; unajijengea tabia ya ushundi na mafanikio; hatua kwa hatua.


SWALI:


*Je, umeshawahi kupanga malengo na ukashindwa kutimiza?* Unadhani tatizo gani lilikukwamisha katika kufikia malengo yako!?




mwandishi : Mrisho Said Mbwembe

                          0657942495

mrishombwembwe@gmail.com

@ BoreshaTanzaniafoundation

Ijumaa, 1 Julai 2022

DHANA YA AKILI NA MAFANIKIO*

 SOMO LA KWANZA


*DHANA YA AKILI NA MAFANIKIO*




📙📙📙📚📚📚📚📙📙📙

Sehemu ya PILI


*Reticular Activating System (RAS) (Mifumo wa Akili wa kuyaendea malengo).*


Kama tulivyosema kawa Akili ina uwezo na mchango mkubwa Sana katika maendeleo na mafanikio yetu; kitu kinachotakiwa ni sisi kujua uwezo huo na kuufanyia kazi.


Kwenye Ubongo Kuna sehemu iitwayo *Reticular Cortex* ambayo hutengeneza mfumo uitwao *Reticular Activating System (RAS)*. Kazi kuu ya RAS ni kuchuja taarifa na kuratibu namna ya kuweka umakini katika Mambo mbalimbali, kwa kuwa ubongo hufanya kazi kwa mahesabu na kuweka vipaumbele!


Kwa mfano; unapokuwa kwenye mashine ya ATM unataka kufanya muamala; ni rahisi Sana kuikumbuka namba yako ya SIRI ya ATM ingawa ukitoka hapo huwa hauitilii umuhimu kabisaa! Unajua kwanini!? *Ni kwa sababu RAS hutusaidia kuwa makini na Jambo Kama tumeandaa mazingira na tumeamua kulifanya*. Hivyo kila fursa unayoamua kuiendea RAS inakudaidia kuweka mazingira vizuri ili uweze kuwa makini nayo na ufanikiwe.


Leo hii ukiamua kufanya biashara ya kuuza Chakula, Batiki, Nguo za kike, Biriani, Kuku au shughuli yoyote ile; utashangaa kuona unaanza kupata watu au wadau mbalimbali wanaojihusisha na shughuli hizo au wanaohitaji kununua, ingawa kabla ya wazo hilo, ulikuwa huwaoni watu hao. Hivyo, RAS katika ubongo hukusaidia kupata watu na taarifa sahihi kuhusu Jambo unalotaka kulifanya.


Kwa ujumla huwezi kupata watu sahihi au taarifa Muhimu za Jambo fulani hadi uweke malengo na kuamua kulifanya Jambo hilo. Unapoweka lengo na kuanza kulifanyia kazi maana yake unaiambia *Reticular Activating System* iwe tayari kukusaidia kutimiza lengo hilo; kwa kuwa Mwenyezi-Mungu ameitengeneza sehemu hiyo kwa kazi hiyo tu!


Watu wote wanaotimiza malengo yao kwa haraka na kwa mafanikio makubwa huwa wanajenga sifa ya:

- *Kujua wanachokifanya*

- *Kufanya kile wanachokipenda*

- *Kuwa na nia isiyoyetereka* n

- *Kutokata tamaa.*

- *Kuwa karibu na watu sahihi wenye malengo yanayofanana* na

- *Kuendelea kujifunza kila siku*


Jambo kuu hapa ni kuamua kufanya Jambo, shughuli au biashara unayoijua na kuipenda toka moyoni. Utashangaa kuona unapata mafanikio makubwa kwa kuwa Akili hukusaidia kufikia malengo yako.

Usifanye Jambo kwa kufuata mkumbo wala usiache ndoto yako kwa kukatishwa tamaa; jua unachokifanya.


Somo litaendelea kwa uweza wa Mwenyezi-Mungu.


*Naomba utoe ushuhuda kuhusu dhana hii ya RAS Kama umeshawahi kuona uhalisia wake kwenye maisha yako* Kama Kuna swali au maoni weka comment hapa chini.




mwandishi : Mrisho Said Mbwembe

0657942495

mrishombwembwe@gmail.com

@ BoreshaTanzaniafoundation