SOMO LA KWANZA
*DHANA YA AKILI NA MAFANIKIO*
📙📙📙📚📚📚📚📙📙📙
Sehemu ya TATU
*Ijue PREFRONTAL CORTEX; sehemu CHANYA ya Akili inayopambana na nguvu HASI (LIMBIC SYSTEM)*
Naendelea kusisitiza kuwa *Ametukuka Mwenyezi-Mungu; mbora wa kuumba*! Katika sehemu ya mbele ya ubongo wa mwanadamu; Kuna sehemu inayoitwa *Prefrontal Cortex*; hii ni sehemu CHANYA inayosimamia mafanikio makubwa ya mwanadamu. Ili kuifahamu vizuri sehemu hii ni vizuri tukajua upande HASI *(LIMBIC SYSTEM)*.
*LIMBIC SYSTEM*
Hii ni sehemu iliyo maeneo ya paji la uso. Huu ni mfumo hasi unaomfanya mwanadamu:
- Awe mvivu
- Apende starehe
- Asipende kujihangaisha
- Akate tamaa mapema
- Aghairishe Mambo muhimu
- Asione umuhimu kusonga mbele n.k.
Mfumo huu unazalisha kemikali iitwayo *Dopermine* (inayozalishwa na Amygdala) ambayo humfanya mwanadamu Apende kuliwazwa na asipende kabisa kujituma. Umeshawahi kuona Alfajir unataka kuamka lakini kuna kitu kinakubembeleza na kukwambia uendelee kulala!? *Hiyo ndiyo kazi inayofanywa na Limbic system*. Hiki ni kilevi. Kwa bahati mbaya; mfumo huu Mwenyezi-Mungu Amauumba ukiwa kamili kwa 100% tangu Mtoto anapozaliwa!
*PREFRONTAL CORTEX*
Ili kudhibiti nguvu ya Limbic system; Mwenyezi-Mungu Ametuwekea sehemu hii CHANYA ya Prefrontal Cortex. Mfumo huu huwa hauko kamili kimaumbile; huwa inakuwa kadiri mwanadamu anavyojitahidi kupambana na nguvu HASI. Kwa hiyo; jinsi unavyozidi kufanya Mambo ya kimaendeleo na kujituma; mfumo huu unakua na Limbic system hupungua nguvu. Unapoweka malengo makubwa na kuanza kuchukua maamuzi makubwa; unajijengea tabia ya ushundi na mafanikio; hatua kwa hatua.
SWALI:
*Je, umeshawahi kupanga malengo na ukashindwa kutimiza?* Unadhani tatizo gani lilikukwamisha katika kufikia malengo yako!?
mwandishi : Mrisho Said Mbwembe
0657942495
mrishombwembwe@gmail.com
@ BoreshaTanzaniafoundation



.jpg)






