Lebo

Jumapili, 28 Agosti 2022

MADA ZA MALEZI NA MAHUSIANO YA KIJAMII.


SOMO: ```MALEZI YA KIMKAKATI.``` 


📗📗📗📗📗📗📗📗📗



🤽🏻‍♂️Kijana mmoja aliomba kazi ya umeneja katika kampuni moja. Alifaulu mahojiano ya awali, na kupata nafasi ya kukutana na Mkurugenzi kwa mahojiano ya mwisho.


Siku ya Mahojiano Mkurugenzi aliuliza,


 ```"Je, ulipata ufadhili wowote wa shule?" kijana akajibu "hapana". "Baba yako ndiye aliyekulipia ada ya shule?"

"Baba yangu alifariki nikiwa na mwaka mmoja, mama yangu ndiye alinilipia karo ya shule," alijibu.``` 


 ✒ "Mama yako anafanya kazi wapi?" "Mama yangu anafanya kazi ya kufua nguo." Mkurugenzi alimwomba kijana aoneshe mikono yake. Kijana akaonesha jozi ya mikono ambayo ilikuwa laini na kamilifu. "Je, umewahi kumsaidia mama yako kufua nguo kabla?" Mkurugenzi alihoji.


😭 _“Kamwe, mama yangu sikuzote alitaka nijifunze na kusoma vitabu zaidi. Isitoshe, mama yangu anaweza kufua nguo haraka kuliko mimi._ 


💡 ```Mkurugenzi akasema, “Nina ombi. Ukienda nyumbani leo, nenda ukasafishe mikono ya mama yako, kisha tuonane kesho asubuhi.

Kijana aliona kuwa nafasi yake ya kupata kazi ilikuwa kubwa. Aliporudi nyumbani, alimwomba mama yake amruhusu kusafisha mikono yake. Mama yake alijisikia furaha lakini akiwa na hisia mchanganyiko, alinyoosha mikono ili kijana aisafishe.


Kijana alisafisha mikono ya mama yake polepole. Chozi lilidondoka kila alivyoendelea kuisafisha mikono ya mama yake. Ilikuwa ni mara ya kwanza kuona mikono ya mama yake ilikuwa imekunjamana sana, na kulikuwa na michubuko mingi mikononi mwake. Michubuko mingine ilikuwa inauma na mama yake alihisi maumivu kila ilipoguswa.``` 


Hii ilikuwa mara ya kwanza kwa kijana huyo kutambua kwamba ni jozi hii ya mikono ndiyo inayofua nguo kila siku ili kumwezesha kulipa karo ya shule. Michubuko katika mikono ya mama ilikuwa ndiyo malipo ya elimu yake na hata maisha aliyonayo.


Baada ya kusafisha mikono ya mama yake, kijana huyo alifua nguo zote zilizokuwa zimebaki. Usiku huo, mama na mwana walizungumza kwa muda mrefu sana. Asubuhi iliyofuata, kijana alienda ofisini kwa mkurugenzi.


Mkurugenzi aliona machozi katika macho ya kijana huyo, akamuuliza: "Je, unaweza kuniambia ni nini umefanya na kujifunza kwa tukio la jana nyumbani kwenu?"


Kijana akajibu, "Nilisafisha mikono ya mama, na pia nikamaliza kufua nguo zote zilizokuwa zimebaki." "Sasa najua na nathamini hili. Bila mama yangu, nisingekuwa hivi nilivyo leo. Kwa kumsaidia mama yangu, sasa ninatambua jinsi ilivyo vigumu na ngumu kufanya kitu peke yako. Na nimekuja kufahamu umuhimu na thamani ya kusaidia familia.


Mkurugenzi alisema, “Hiki ndicho ninachotafuta kwa meneja. Ninataka kuajiri mtu ambaye anaweza kuthamini msaada wa wengine, mtu anayejua mateso ya wengine ili kufanya mambo, na mtu ambaye hawezi kuweka pesa kuwa lengo lake pekee maishani.”


 “Umeajiriwa.”


Kijana huyu alifanya kazi kwa bidii sana, na akapokea heshima ya wasaidizi wake. Kila mfanyakazi alifanya kazi kwa bidii na alifanya kazi kama timu. Utendaji wa kampuni uliimarika sana.

Mtoto, ambaye amelelewa kwa kudekezwa akipewa chochote anachotaka kamwe hujiweka kwanza kwa kila jambo na kila wakati. Anakuwa hajui juhudi za mzazi wake. 


Anapoanza kazi, anafikiri kwamba kila mtu lazima amsikilize, na anapokuwa meneja, hatajua mateso ya wafanyakazi walio chini yake na daima atakuwa mtu wa kulaumu wengine. Kwa watu wa aina hii, ambao wanaweza kuwa wazuri kielimu, wanaweza kufaulu kwa muda.

Watanung'unika na kujaa chuki na kupigania zaidi. Ikiwa sisi ni wazazi wa aina hii wanaolinda, je, kweli tunaonesha upendo au tunaharibu watoto wetu? Unaweza kumruhusu mtoto wako aishi katika nyumba kubwa, kula chakula kizuri, kujifunza kuogelea, kutazama mpira (sijui timu gani). 


Lakini unapokata nyasi, tafadhali waruhusu wapate uzoefu. Baada ya chakula, acha waoshe sahani na bakuli zao pamoja na ndugu na dada zao. Sio kwa sababu huna pesa za kuajiri mjakazi, lakini ni kwa sababu unataka kuwapenda kwa njia sahihi. 


Unataka waelewe, hata wazazi wao wawe matajiri kiasi gani, siku moja nywele zao zitakua mvi, sawa na mama wa huyo kijana. Jambo muhimu zaidi ni kwamba mtoto wako anajifunza jinsi ya kuthamini juhudi na uzoefu wa ugumu na kujifunza uwezo wa kufanya kazi na wengine ili kufanya mambo.


AKILI YA MAFANIKIO


📘📘📘📘📘📘📘📘📘

Ijumaa, 8 Julai 2022

DHANA YA AKILI NA MAFANIKIO

 SOMO LA KWANZA


*DHANA YA AKILI NA MAFANIKIO*


📙📙📙📚📚📚📚📙📙📙


Sehemu ya TATU 


*Ijue PREFRONTAL CORTEX; sehemu CHANYA ya Akili inayopambana na nguvu HASI (LIMBIC SYSTEM)*





Naendelea kusisitiza kuwa *Ametukuka Mwenyezi-Mungu; mbora wa kuumba*! Katika sehemu ya mbele ya ubongo wa mwanadamu; Kuna sehemu inayoitwa *Prefrontal Cortex*; hii ni sehemu CHANYA inayosimamia mafanikio makubwa ya mwanadamu. Ili kuifahamu vizuri sehemu hii ni vizuri tukajua upande HASI *(LIMBIC SYSTEM)*.


*LIMBIC SYSTEM*



Hii ni sehemu iliyo maeneo ya paji la uso. Huu ni mfumo hasi unaomfanya mwanadamu:

- Awe mvivu

- Apende starehe

- Asipende kujihangaisha

- Akate tamaa mapema

- Aghairishe Mambo muhimu

- Asione umuhimu kusonga mbele n.k.

Mfumo huu unazalisha kemikali iitwayo *Dopermine* (inayozalishwa na Amygdala)  ambayo humfanya mwanadamu Apende kuliwazwa na asipende kabisa kujituma. Umeshawahi kuona Alfajir unataka kuamka lakini kuna kitu kinakubembeleza na kukwambia uendelee kulala!? *Hiyo ndiyo kazi inayofanywa na Limbic system*. Hiki ni kilevi. Kwa bahati mbaya; mfumo huu Mwenyezi-Mungu Amauumba ukiwa kamili kwa 100% tangu Mtoto anapozaliwa!


*PREFRONTAL CORTEX*

Ili kudhibiti nguvu ya Limbic system; Mwenyezi-Mungu Ametuwekea sehemu hii CHANYA ya Prefrontal Cortex. Mfumo huu huwa hauko kamili kimaumbile; huwa inakuwa kadiri mwanadamu anavyojitahidi kupambana na nguvu HASI. Kwa hiyo; jinsi unavyozidi kufanya Mambo ya kimaendeleo na kujituma; mfumo huu unakua na Limbic system hupungua nguvu. Unapoweka malengo makubwa na kuanza kuchukua maamuzi makubwa; unajijengea tabia ya ushundi na mafanikio; hatua kwa hatua.


SWALI:


*Je, umeshawahi kupanga malengo na ukashindwa kutimiza?* Unadhani tatizo gani lilikukwamisha katika kufikia malengo yako!?




mwandishi : Mrisho Said Mbwembe

                          0657942495

mrishombwembwe@gmail.com

@ BoreshaTanzaniafoundation

Ijumaa, 1 Julai 2022

DHANA YA AKILI NA MAFANIKIO*

 SOMO LA KWANZA


*DHANA YA AKILI NA MAFANIKIO*




📙📙📙📚📚📚📚📙📙📙

Sehemu ya PILI


*Reticular Activating System (RAS) (Mifumo wa Akili wa kuyaendea malengo).*


Kama tulivyosema kawa Akili ina uwezo na mchango mkubwa Sana katika maendeleo na mafanikio yetu; kitu kinachotakiwa ni sisi kujua uwezo huo na kuufanyia kazi.


Kwenye Ubongo Kuna sehemu iitwayo *Reticular Cortex* ambayo hutengeneza mfumo uitwao *Reticular Activating System (RAS)*. Kazi kuu ya RAS ni kuchuja taarifa na kuratibu namna ya kuweka umakini katika Mambo mbalimbali, kwa kuwa ubongo hufanya kazi kwa mahesabu na kuweka vipaumbele!


Kwa mfano; unapokuwa kwenye mashine ya ATM unataka kufanya muamala; ni rahisi Sana kuikumbuka namba yako ya SIRI ya ATM ingawa ukitoka hapo huwa hauitilii umuhimu kabisaa! Unajua kwanini!? *Ni kwa sababu RAS hutusaidia kuwa makini na Jambo Kama tumeandaa mazingira na tumeamua kulifanya*. Hivyo kila fursa unayoamua kuiendea RAS inakudaidia kuweka mazingira vizuri ili uweze kuwa makini nayo na ufanikiwe.


Leo hii ukiamua kufanya biashara ya kuuza Chakula, Batiki, Nguo za kike, Biriani, Kuku au shughuli yoyote ile; utashangaa kuona unaanza kupata watu au wadau mbalimbali wanaojihusisha na shughuli hizo au wanaohitaji kununua, ingawa kabla ya wazo hilo, ulikuwa huwaoni watu hao. Hivyo, RAS katika ubongo hukusaidia kupata watu na taarifa sahihi kuhusu Jambo unalotaka kulifanya.


Kwa ujumla huwezi kupata watu sahihi au taarifa Muhimu za Jambo fulani hadi uweke malengo na kuamua kulifanya Jambo hilo. Unapoweka lengo na kuanza kulifanyia kazi maana yake unaiambia *Reticular Activating System* iwe tayari kukusaidia kutimiza lengo hilo; kwa kuwa Mwenyezi-Mungu ameitengeneza sehemu hiyo kwa kazi hiyo tu!


Watu wote wanaotimiza malengo yao kwa haraka na kwa mafanikio makubwa huwa wanajenga sifa ya:

- *Kujua wanachokifanya*

- *Kufanya kile wanachokipenda*

- *Kuwa na nia isiyoyetereka* n

- *Kutokata tamaa.*

- *Kuwa karibu na watu sahihi wenye malengo yanayofanana* na

- *Kuendelea kujifunza kila siku*


Jambo kuu hapa ni kuamua kufanya Jambo, shughuli au biashara unayoijua na kuipenda toka moyoni. Utashangaa kuona unapata mafanikio makubwa kwa kuwa Akili hukusaidia kufikia malengo yako.

Usifanye Jambo kwa kufuata mkumbo wala usiache ndoto yako kwa kukatishwa tamaa; jua unachokifanya.


Somo litaendelea kwa uweza wa Mwenyezi-Mungu.


*Naomba utoe ushuhuda kuhusu dhana hii ya RAS Kama umeshawahi kuona uhalisia wake kwenye maisha yako* Kama Kuna swali au maoni weka comment hapa chini.




mwandishi : Mrisho Said Mbwembe

0657942495

mrishombwembwe@gmail.com

@ BoreshaTanzaniafoundation

Jumamosi, 25 Juni 2022

Ijumaa, 24 Juni 2022

UPDATE KUHUSU AJIRA MPYA ZA WALIMU NA WATUMISHI WA KADA YA AFYA


 Waziri wa Tamisemi  MHE. INNOCENT BASHUNGWA amesema kuwa wiki hii wanatarajia kutangaza ajira mpya za walimu pamoja na watumishi WA KADA ya Afya. 

Waziri ameyasema hayo akiwa katika mkutano na wadau mbalimbali uliofanyika kupitia zoom wakijadiri kuhusu zoezi la uwekaji alama za mipaka tarafa ya Loliondo na maendeleo ya zoezi la uhamaji wa hiari kwa wakazi wa Ngorongoro 

Kuangalia video ya mkutano huo bofya hapo chini 







Jumamosi, 18 Juni 2022

SILSILA YA MASOMO YA AKILI YA MAFANIKIO


MADA 


DHANA YA AKILI

SEHEMU YA KWANZA


Neno AKILI (Mind or Intellect) ni tofauti kimaana na neno UBONGO (Brain); ingawa watu wengi hudhani kuwa maneno haya mawili yana maana moja, la hasha wa kalla!


Kwa kuanzia; neno UBONGO linamaanisha Ogani kubwa iliyohifadhiwa kwenye fuvu la kichwa. Ogani au umbile hili limeundwa na vitu kadhaa ambavyo ni:

- Nyamanyama laini

- Mishipa ya damu (Blood vessels)

- Mishipa ya fahamu (Nerves)

- Chembechembe za damu (Blood cells)

- Tishu (Tissues) mbalimbali na

- Majimaji (Waterly Fluids).

Ubongo umegawanyika katika maeneo makuu matatu ambayo ni:

1. Ubongo wa mbele (Frontal Brain)

2. Ubongo wa kati (Mid brain)

3. Ubongo wa nyuma (Hind brain) ambao unaungana na uti wa mgongo kupitia Medulla Oblongata.



AKILI

Kwa upande wa pili; AKILI ni uwezo uliopo kwenye ubongo unaomuwezesha mwanadamu kuweza kutafakari, kuchambua, kupima, kuchanganua na kutafuta ufumbuzi wa mambo mbalimbali yanayomzunguka.


Ni vigumu kujadili suala lolote la mafanikio na maendeleo bila ya kuhusisha Akili. Labda tuseme kuwa Mafanikio yoyote huanzia kwenye akili ya mtu. ambazo Mwenyezi-Mungu anaziongoza; ndiyo maana wengine husema kuwa, " Man is the product of his own mind.(Mtu ni zao la AKILI yake mwenyewe). Vilevile; James Allen katika kitabu chake cha As the man thinketh anasema wazi kuwa;


"Wewe ni matokeo ya mawazo yanayozunguka akilini mwako kila wakati."; yaani, "You are the product of your dominant thoughts."


Hata katika imani ya dini tunafundishwa kuwa Mwenyezi-Mungu amemfanya mwanadamu kuwa mtawala na kiongozi ( Khalifa ) kwa kumpa uwezo mkubwa wa Akili tofauti na viumba wengine. Kwa hiyo; Mafanikio na maendeleo yote ya mwanadamu na jamii yake kwa ujumla huanzia AKILINI. 


Katika Akili kuna nguvu kuu aina tatu ambazo zinaleta mafanikio makubwa Sana: Kama ukizijua na kuanza kuzifanyia kazi; Je, unataka kuzijua nguvu hizo!!?............


Naam; nguvu hizo ni:


1. Reticular Activating System (Mfumo wa Akili wa kuyaendea malengo)


2. Prefrontal Cortex System (Mfumo wa Akili wa kupambana na hisia hasi)


3. Subconscious mind (Akili nusu razini).


Tutazielezea hizi kwenye somo linalofuata Mwenyezi-Mungu Akipenda.


Somo litaendelea......




mwandishi : Mrisho Said Mbwembe

0657942495

mrishombwembwe@gmail.com

@ BoreshaTanzaniafoundation

KAA TAYARI


Mfululizo wa masomo yanayohusu AKILI NA MAFANIKIO " yataanza hii leo juma mosi na mada zitaendelea kila inapofika juma mosi na juma tano kaa tayari







mwandishi : Mrisho Said Mbwembe

0657942495

mrishombwembwe@gmail.com

@ BoreshaTanzaniafoundation

Jumatatu, 13 Juni 2022

SIX LEADERSHIP PRINCIPLES TO LEARN FROM AN EAGLE



1. Eagles fly Alone and at High Altitudes.

They don't fly with sparrows, ravens, and other small birds.


MEANING; Stay away from narrow-minded people, those that bring you down. Eagle flies with Eagles. Keep good company.



2. Eagles have an Accurate Vision. 

They have the ability to focus on something as far as 5km away. No matter the obstacles, the eagle will not move his focus from the prey until he grabs it.


MEANING; Have a vision and remain focused no matter what the obstacles and you will succeed.



3. Eagles do not Eat Dead things

They Feed only on Fresh Prey.


MEANING; Do not rely on your past success, keep looking for new frontiers to conquer. Leave your past where it belongs, in the past.




4. Eagles Love the Storm.

When clouds gather, the eagle gets excited, the eagle uses the storms wind to lift itself higher. Once it finds the wind of the storm, the eagle uses the raging storm to lift itself above the clouds. This gives the eagle an opportunity to glide and rest its wings. In the meantime, all the other birds hide in the branches and leaves of the tree.


MEANING; Face your challenges head on knowing that these will make you emerge stronger and better than you were. We can use the storms of life to rise to greater heights. Achievers are not afraid to rise to greater heights. Achievers are not afraid of challenges, rather they relish them and use them profitably.


5. Eagles Prepare for Training;

They remove the feathers and soft grass in the nest so that the young ones get uncomfortable in preparation for flying and eventually flies/ when it becomes unbearable to stay in the nest./


MEANING; Leave your Comfort Zone, there is No Growth there.




6. When the Eagle Grows Old,

His feathers becomes weak and cannot take him as fast and as high as it should. This makes him weak and could make him die. So he retires to a place far away in the mountains. While there, he plucks out the weak feathers on his body and breaks its beaks and claws against the rocks until he is completely bare; a very bloody and painful process. Then he stays in this hiding place until he has grown new feathers, new beaks and claws and then he comes out flying higher than before.


MEANING; We occasionally need to shed off old habit no matter how difficult, things that burden us or add no value to our lives should be let go of.



Never give up. Be an Eagle.